Wednesday, 31 May 2017

TUIUNGENI MKONO COMBINE YA ROLLING STONE,RAZA LEE.

Mdau wa michezo visiwani Zanzibar Mohamed Ibrahim “Raza Lee”amewataka wadau mchezo wa mpira wa miguu visiwani Zanzibar kuungana kwa hali na mali kuwapatia vifaa sambamba na michango yao timu ya Combine ya wilaya ya mjini inayotarajiwa kushiriki katika mashindano ya Rolling stone yatakayofanyika kuanza June 29, 2017 hadi July 9, 2017 jijini Arusha.
Mdau wa soka Visiwani Zanzibar Mohamed Ibrahim "Raza Lee"akikabidhi mipira kwa viongozi wa combine ya rolling stone wa kat ni katibu wa timu hiyo Ali Othman na kocha Muhamed Seif King.(Picha na Abubakary Hatibu)


Akizungumza na zenjsport-on line mara baada yakukabidhi vifaa hivyo mdau huyo wa michezo visiwani amesema ipo haja yakuwaunga mkono vijana hao ambao wamepania kurudi na ushindi katika mashindano hayo.

Ameongeza kuwa endapo wadau wa soka watatoa michango yao ya hali na mali imani yake vijana hao watafanya vyema katika mashindano hayo.


Timu ya combine ya wilaya ya mjini wanakwenda katika mashindano hayo kutetea taji lao walilotwaa katika mashindano yaliyofanya mwaka jana Arusha Tanzania.

No comments:

Post a Comment