Timu kongwe
katika historia ya soka la Zanzibar na vinara wa ligi kuu soka ya Zanzibar
iliyopo katika hatua ya nane bora timu ya Jamhuri wamepania kuhakikisha watwaa
ufalme wa soka nakuiwakilisha nchi kimataifa.
Jamhuri
ambao wamefanikiwa kujinyakulia alama tisa katika michezo mitatu iliyocheza kabla
yakuingia mapumzikoni kupisha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani inaendelea
na maandalizi kwa ajili ya ligi hiyo inayotarajiwa kuendelea tena July 9 ,mwaka
huu.
![]() |
Kocha wa vinara wa ligi kuu soka ya Zanzibar Abdulmutik Haji |
Kwa mujibu
wa taarifa iliyotolewa na kocha mkuu wa timu hiyo Abdumutik Haji imesema wanajipanga
kuona wanamaliza ligi hiyo wakiwa vinara nakujinyakulia tiketi yakuiwakilisha
nchi kimataifa.
“Unajua mimi
naijua vizuri ligi ya Zanzibar pia vijana wangu wapo vizuri tunajianda kupambana ili kutwaa taji la ubingwa wa Zanzibar ,jambo ambalo linawezekana sana tu,tumeanza vizuri michezo hii ya hatua ya nane bora najua vijana wangu hawataniangusha ”alisema.
Ameongeza
kuwa kasi ambayo kikosi chake hicho imeianza nayo katika ligi hiyo itaendelea
nayo na imani yake kubwa nikufanya vyema kutokana na nyota ambao wapo katika
kikosi chake wana ari yakujituma kufanya vyema katika michezo hiyo ya ligi kuu
iliyosalia.
Akizungumzia
soka la kisiwa cha Unguja na Pemba kocha huyo amesema hakuna tofauti kubwa timu
za pande zote mbili zinalingana kinachopelekea timu za Pemba kuharibu katika
misimu iliyopita ni maandalizi duni jambo ambalo katika kikosi chake kwa msimu huu halipo.
Jamhuri
itaendelea kutafuta heshima yake July ,10 ambapo itakuwa mgeni wa timu ya
Zimamoto mtanange ambao utavurumishwa katika uwanja wa Amani mnamo majira ya
saa kumi alasiri.
No comments:
Post a Comment