Mshambuliji wa Miembeni City aliyepo katika kikosi cha
Combine ya wilaya ya mjini Ibrahim Abdallah(Imu Mkoko) amesema anamatumaini
makubwa ya kikosi hicho kutwaa tena taji hilo.
![]() |
Mshambuliji wa timu ya Miembeni City Ibrahim Abdallah akiwa katika mazoezi ya combine ya Rolling Stone. |
Mkoko ameyasema hayo wakati alipokuwa akizungumza na
mwandsihi wa habari hizi nakusema kuwa kutokana na uwezo wa wachezaji waliopo
katika kikosi hicho sambamba na ari iliyopo anaimani wataibuka kidedea katika
michezo hiyo.
“Nimeona wachezaji wote waliopo katika kikosi kile wanauwezo
wa hali ya juu hivyo imani yangu tutaenda kupambana na kutetea taji ambalo
tulitwaa katika mashindano yaliyopita kikubwa tunawaomba Wazanzibar watuombe ilitukafanye kile ambacho wanakihitaji “alisema mshambuliji huyo.
Akizungumzia ujio wa kiungo wa Kilimani City Asaad Juma Deco ambae walikuwepo pamoja katika kikosi cha Serengeti Boys ,Mkoko amesema kuwa ujio wa nyota huyo unazidi kuamsha ari katika kikosi hicho huku akisema kuwa mwalimu ameongeza mtu sahihi kwani kutokana na uzoefu alonao utasaidia kuimarisha uimara katika kikosi hicho.
![]() |
MKOKO AKIWAJIBA KATIKA KIKOSI CHA SERENGETI BOYS. |
Mkoko ambae amejiunga na kikosi hicho wiki hii akitokea Gabon
katika mashindano ya mataifa ya Afrika kwa timu za vijana akiwa na Serengeti
boys ameongeza kuwa juhudi na ari iliyopo kwa nyota wenzake sambamba na utayari
wa viongozi bila shaka utaisaidia timu hiyo kuibuka ushindi katika michezo
hiyo.
Mashindano ya Rolling Stone inaendelea na mazoezi yake kujiandaa na
mashindano hayo yanayotarajiwa kuanza kuanzia June 29 Jiji Arusha.
No comments:
Post a Comment