Tuesday, 25 July 2017

Fii akosa penalt ,boys yalala kwa fire.

Timu ya Zimamoto imefanikiwa kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Jang’ombe Boys katika mchezo wa ligi kuu soka ya Zanzibar hatua ya 8 bora uliosukumwa jioni ya leo katika uwanja wa Amaan.
Mchezaji wa Jang'ombe Boys Fii akijiandaa kupiga Penalt.

Goli la Zimamoto lilifungwa na Idrissa Simai Pandu dakika ya 84.
Katika mchezo huo mlinzi wa kati wa Jang'ombe boys Ali Humud Badri (Balii) alitolewa nje kwa kadi njekundu baada yakuunawa kwa makusudi mpira uliokuwa ukimpita.
Wachezaji wa timu ya Zimamoto wakilalamikia maamuzi ya muamuzi Haule.

Mchezo mwengine umepigwa katika uwanja wa Gombani kisiwani Pemba timu ya Jamhuri ikaenda sare ya 1-1 dhidi ya Okapi.
Kocha wa timu ya Jang'ombe boys Muhamed akisalimiana na Fii.

Bao la Okapi limefungwa na Bakar Hamad dakika ya 5 wakati bao la Jamhuri limefungwa na Ahmed Ali Omar dakika ya 20.

PICHA TOFAUTI JANG'OMBE BOYS VS FIRE











No comments:

Post a Comment