Wednesday, 26 July 2017

NYOTA GULION FC ASAINI MIAKA MIWILI STAND UNITED.

Mlinzi wa kati wa timu ya Gulion FC Ali Hamad Ali inayoshiriki ligi daraja la pili wilaya ya mjini Unguja amesajili miaka mkataba wa miaka miwili kuitumikia timu ya Stand United ya Tanzania bara.
Ali Hamad Ali akizungumza na waandishi wa habari.

Akizungumza na mtandao huu nyota huyo ameelezea kufurahishwa kwake nakusajiliwa na timu hiyo huku akisema kuwa hiyo itakuwa safari yake yakuanzia kucheza soka lakulipwa.

Amesema kuwa atahakikisha anajituma kwa hali na mali kuhakikisha anakiimarisha kiwango chake ulikufanikisha malengo yake.


Ali Hamad Ali ameanza soka lake katika timu ya Vikokotoni tokea madaraja ya vijana kabla yakujiunga timu ya Gulion akiwa nahodha wa timu hiyo.

No comments:

Post a Comment