Saturday, 5 August 2017

Nikimuona Hilika uwanjani namkumbuka Said Mwamba Kizota ,kocha Shekha.

Aliyekuwa nahodha wa timu ya taifa ya Zanzibar katika miaka ya 90 Shekha Khamis ameelezea kufurahishwa na uwezo alionao mshambuliaji wa timu ya Zimamoto inayoshiriki ligi kuu soka ya Zanzibar.
Mshambuliaji wa timu ya Zimamoto Ibrahim Hamad Hilika alievaa jezi manjano akijaribu kumtoka Feisal Salum wa JKU.

Kocha Shekha ameyasema hayo wakati alipokuwa akizungumza na mtandao huu nakusema aina ya uchezaji alionao Hilika unaenda na washambuliaji waliokuwepo katika kipindi ambacho yeye akicheza soka.

Amesema anapomuona nyota huyo akiwa uwanjani anamfananisha na Said Mwamba Kizota ambae alikuwa mshambualiji hatari sana katika kipindi ambacho yeye akicheza soka.

Ameongeza kuwa endapo nyota huyo ataendeleza kiwango chake alichonacho kutasamsaidia kufika mbali zaidi kisoka.

Kocha Shekha alikuwa nahodha wa timu ya taifa ya Zanzibar iliyotwaa ubingwa katika mashindano ya Challenge mwaka 1995.


No comments:

Post a Comment