Chama cha mpira
wa miguu visiwani kimekutana na vilabu vinavyoshiriki ligi kuu soka ya Zanzibar
kanda ya Unguja kupanga mikakati kadhaa yakufanikisha msimu ujao wa ligi.
Katika kikao
hicho kilichofanyika asubuhi ya leo katika kiwanja cha Amani pamoja na mambo
mengine vilabu pamoja na ZFA wamekubaliana kuanza kwa msimu ujao October mwaka
huu.
Sambamba na
hayo vilabu vimetakiwa kuendelea na zoezi la usajili na uhamisho huku wakisisitizwa
kulipia ada ya mashindano,ada ya mwaka kwa mrajisi wa vyama vya michezo
sambamba na ada ya mwaka katika wilaya ambapo kila inatoka.
Akizungumza na
viongozi wa vilabu 14 vinavyoshiriki ligi kuu soka ya Zanzibar kanda ya Unguja
rais wa chama cha mpira wa miguu visiwani Ravia Idarous amesema katika msimu
ujao wa ligi hawataziruhusu kushiriki katika mashindano timu ambazo hazijalipia
ada ya mashindano sambamba na ada zote ambazo vilabu vinatakiwa kulipa.
Ameongeza kuwa
malipo yote hayo yanatakiwa kufanywa kupitia akauti ya ZFA iliyopo bank ya watu
wa Zanzibar na baada yakulipia ada hizo wanatakiwa kufikisha ofisini risiti huku
akisisitiza kuwa hakuna pesa itakayopokelewa mkononi.
Amewataka
viongozi wa vilabu kufanya usajili katika kipindi kilichowekwa na chama chao
hakitaongeza siku za usajili.
Kuhusu mfumo
ambao utatumika kwa ajili ya msimu ujao wa ligi amesema utaendelea mfumo ule
ule wa mwaka jana huku vilabu vikitakiwa kudumisha nidhamu katika michezo hiyo.
Vilabu 14
ambavyo vitashiriki ligi kuu soka ya Zanzibar kanda ya Unguja ni Chuoni,Blacksaloir,KVZ,KMKM,Mafunzo,Zimamoto,JKU,Kilimani
City,Jang’ombe Boys,Taifa ya Jang’ombe,Kipanga, Charawe na Miembeni City.
No comments:
Post a Comment