Baada ya kipigo cha magol 2-0 kutoka kwa mabingwa wa
ligi kuu soka ya Zanzibar timu ya Miembeni City inatarajiwa kuingia kambini
jioni ya leo September 20 kujiandaa na ligi kuu soka ya Zanzibar kituo cha Unguja inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi lake
October 3 mwaka huu.
KIKOSI CHA MIEMBENI CITY KILICHOANZA KATIKA MCHEZO WA NGAO YA HISANI DHIDI YA JKU |
Miembeni City ambao walipokea kipigo hicho katika
mchezo wa Ngao ya Hisani uliovurumishwa jioni ya jana katika dimba la Amani
mjini Unguja wameaamua kukaa kambi ilikupata muda wakutosha wakukiandaa kikosi
hicho kuelekea msimu mpya wa ligi.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya timu hiyo
vijana hao wanatarajiwa kuingia kambini jioni ya leo na hawatatoka hadi siku ya
mchezo wao wa kwanza wa ligi kuu dhidi ya Polis mchezo ambao unatarajiwa
kusukumwa katika kiwanja cha Amani mjini Unguja October 5 mnamo majira ya saa
kumi alasiri.
No comments:
Post a Comment