Timu ya
Dulla Boys ya Jambiani wilaya ya kusini
Unguja kesho inatarajiwa kupiga mchezo wa kirafiki na timu ya Combine ya wilaya
ya mjini mtanange ambao utavurumishwa katika kiwanja cha Amani mjini Unguja
mnamo majira ya saa mbili na nusu usiku.
![]() |
Kocha mkuu wa combine ya wilaya ya mjini Muhamed Seif King. |
Mchezo huo
wa kirafiki ni maalum kwa combine ya wilaya ya mjini kujipima nguvu kuelekea
mashindano ya Rolling Stone yanayotarajiwa kufanyika Mbulu Manyara kuanzia July 7 mwaka huu.
Akizungumza na
mtandao huo kocha mkuu wa timu ya combine ya wilaya ya mjini Muhamed Seif King
amesema katika mchezo huo wa kirafiki anatarajiwa kumtumia mshambuliaji wake
hatari Ibrahim Abdallah Mkoko ambae alijiunga na timu hiyo akitokea Gabon
katika mashindano ya AFCON.
Ukiachia
Mkoko kocha huyo amesema kuwa anatarajiwa pia kumtumia mshambuliaji wa timu ya
Villa United Juma Ali Yussuf(James).
![]() |
Wachezaji wa combine ya wilaya ya mjini baada ya mazoezi |
Ameongea kuwa
kikosi hicho kitaendelea kucheza michezo ya kirafiki kila mwezi mara mbili
ilikukieka sawa kikosi chao hicho.
Aidha kocha
King amewataka washabiki na wapenzi wa soka visiwani Zanzibar kujitokeza kwa
wingi katika mchezo huo ilikuona viwango vya vijana wake ambao wamepania
kufanya vyema katika mchezo huo.
No comments:
Post a Comment