Kiungo wa timu
ya Kilimani City Asaad Juma (DECO) ameomba kuondolewa katika kikosi cha Rolling
Stone kinachotarajiwa kushiriki katika mashindano hayo yanayotarajiwa kufanyika
Mbulu Manyara kuanzia July 7 mwaka huu.
![]() |
Kiungo Assad Juma akiwa katika majukumu ya taifa na Serengeti Boys. |
Kwa mujibu
wa taarifa iliyotolewa na kocha mkuu wa timu hiyo Muhamed Seif King imesema
sababu kuu iliyopelekea kuomba kujindoa katika kikosi hicho nikutokana na nyota
huyo kuhitaji kupumzika kutokana nakufanya kazi sana katika timu ya taifa ya
vijana ya Tanzania Serengeti Boys.
“Unajua Ibny
Asaad tulimuita akatukubalia kujiunga na kikosi lakini baada ya mazoezi ya siku
mbili akaomba kupumzika na uongozi umemkubalia nakumpa baraka zote tunamshukuru
ametuheshimu tulipomita katika kikosi chetu”alisema King.
![]() |
Kiungo wa timu ya Kilimani City Asaad Juma akiwa na jezi ya Serengeti Boys. |
Ameongeza kuwa
kumruhusu kuondoka katika kikosi hicho kwa kiungo huyo hakutoathiri chochote
katika kikosi chao hicho na anamatumaini makubwa yakuona kikosi chao kinafanya
vyema katika mashindano hayo.
Kikosi cha
Combine ya wilaya ya mjini kinatarajiwa kuondo visiwani Zanzibar kuelekea Mbulu
Manyara ,Tanzania bara July 4 mwaka huu tayari kwa ajili ya mashindano hayo.
No comments:
Post a Comment