Ikiwa ni siku mbili
tokea kufunguliwa kwa zoezi la usajili na uhamisho visiwani Zanzibar viongozi
wa vilabu vitatu tofauti vimekuwa vikihaha kuihitaji huduma ya kiungo hatari wa
Miembeni City Haroun Abdallah Jabir(Boban)
Kwa mujibu wa taarifa
za ndani ambazo mtandao huu umezinasa tayari vilabu hivi vikubwa kwa sasa
visiwani hapa wameshatuma watu wao kuanza kwa mazungumzo na nyota huyo ambae
alikuwa msaada mkubwa katika timu yake hiyo.
Juhudi zakumpata
kiungo huyo zimepatikana nakuthibitisha kutakiwa na vilabu hivyo vitatu
nakusema yeye yupo tayari kucheza popote pale jambo la msingi ni maslahi yake
sambamba nakufikia makubaliano na timu yake ya sasa ambayo anamkataba nayo wa
miaka mitatu.
Aidha kiungo huyo hatari
wa timu ya Miembeni City ameanza mazoezi madogomadogo yakujieka sawa kwa ajili
ya msimu ujao wa ligi.
Boban ambae yupo
mapumzikoni Tanzania bara ameanza mazoezi hayo mepesi yakujieka sawa tayari kwa
msimu ujao wa ligi katika fukwe za Kibiji jijini Dar es salam.
Akizungumza na mtandao
huo kiungo huyo ambae alikuwa chachu ya mafanikio katika timu yake hiyo amesema
ameamua kuanza mazoezi ilikuuweka sawa mwili wake tayari kwa ajili ya msimu
ujao wa ligi.
Ameongeza kuwa
anajipanga kuona anaisadia timu yake kufanya vyema katika msimu mpya wa ligi
nakufanya vyema zaidi kama walivyofanya msimu uliopita.
No comments:
Post a Comment