Thursday, 11 May 2017

MASHABIKI WA SOKA WATARAJIE MAKUBWA,KISANDU.


Kocha mkuu wa timu ya chuo cha waandishi wa habari Zanzibar Abubakary Hatibu Kisandu amesema vijana wake wapo vizuri kwa ajili ya mashindano ya vyuo vikuu na taasisi ya elimu ya juu Zanzibar yanayotarajiwa kuanza Jumapili May 14 mwaka huu.

Akizungumza na zenjsport on –line kocha huyo amesema vijana wake wapo vizuri na wanaendelea na mazoezi huku kikosi chake cha mwaka huu kimesheheni nyota kadhaa ambao wanauwezo wa hali ya juu katika kusakata soka.

Akiwataja baadhi ya nyota ambao wapo katika kikosi chake ni pamoja na kiungo anaekipiga timu ya Taifa ya Jang’ombe Muhamed Said ‘Messi’,mshambuliaji wa timu ya Polisi Khamis Maulid na nyota kadhaa ambao wanatarajiwa kuonesha kandanda safi katika mashindano hayo.

Kocha wa timu ya Chuo cha uandishi wa habari Abubakary Hatibu alievaa shuti nyeusi akiwa katika picha ya pamoja na nyota wa timu hiyo.

Ameongeza kuwa lengo lake kama mwalimu nikuona timu inachukua ubingwa katika mashindano hayo ambayo katika msimu uliuopita walitolewa katika hatua ya makundi.

Sambamba na hayo Kisandu amesema kuwa uongozi wa chuo umeongeza posho kwa wachezaji ili kumasha ari zaidi nakuifanya timu ifanye vizuri katika mashindano hayo ya Zahilfe Cup.

Katika mashindano yaliyofanyika mwaka jana Chuo cha Uandishi wa habari Zanzibar kilitolewa katika hatua ya makundi baada yakupokea kipigo katika michezo yote ya hatua hiyo ambapo walifungwa na magol 4-0 na Sumait,3-0 na Microtech nakumaliza ka kipigo cha magol 2-1 kutoka kwa timu ya ICPS.


No comments:

Post a Comment