Thursday, 11 May 2017

KAMATI TENDAJI ZFA PEMBA ,YATOA MAAMUZI MAZITO

Anaandika Abdi Suleiman ,Pemba.
ZFA Taifa Pemba Imeiteremsha daraja timu ya Maji Mjai kutoka ligi kuu ya Zanzibar, hadi daraja la kwanza Taifa msimu wa 2017/2018, pamoja na kuitoza faini ya shilingi Milioni 1,200,000/= kwa makosa mawili tafauti.

Kosa la kwanza kwa Timu hiyo katika mchezo wake na Shaba wa Aprili 28 mwaka huu, timu ya Maji Maji ilifika Uwanjani na wachezaji nane tu na
kupekea baadhi ya wachezaji kuanguka uwanjani na kushindwa kuendelea
na mchezo huo.

Kaimu Msaidizi Katibu Mkuu ZFA Taifa Khamis Hamad Juma, alisema baada ya hali hiyo mwamuzi wa mchezo huo alilazimika kulivunja pambano hilo
dakika ya 44, huku Shaba ikiwa inaongoza kwa goli 1-0.
Makamo wa rais wa ZFA Ali Muhamed 

“Kutokana na hali ilivyokuwa uwanjani baada ya wachezaji watatu kuumia, wakabakia wachezaji watano mwamuzi hakuweza kuendelea na
mchezo na kulivuanja pambano”alisema.

Alisema kwa mujibu wa kanuni za kuendeshea mashindano ya Mpira wa Miguu Zanzibar, Kifungu namba 21 (a)(i) timu ya Maji Maji imepoteza
mchezo huo na shaba kuwepwa ushindi, pamoja na kuteremsha daraja la
kwanza Taifa n kwa msimu 2017/2018 na kutozwa faini ya laki 600,000/= faini ambayo inatakiw akulipwa Mei 30 mwaka huu.

Khamis alisema kosa la pili kwa timu hiyo katika mchezo wake na Jamhuri wa Aprili 26 mwaka huu katika uwanja wa FFU Finya, ulishindwa
kumalizika kwa wakati baada ya wachezaji Abrahman Haji Othaman alikuwa na jezi No. 30 c/No. 020, Bakar Said Ginyari Jezi No. 11C/No. 013,
Branka Ali Yassin jezi NO. 9 C/No. 024 na Ibrahim Said Juma jezi No.17.

Wachezaji hao walidaiwa kumpiga mwamuzi Seif Kesi na kumsababishia maumivu makali pamoja na kupoteza vifaa vyake alivyokuwa akitumia kwa
ajili ya maamuzi anapokuwa kiwanjani na kushindwa kabisa kuendelea
kuchezesha mchezo.

Alisema kwa mujibu wa kanuni ya mashindano kifungu namba 26 C(1), Maji Maji imepoteza mchezo huo na kupewa timu ya Jamhuri, huku wachezaji
hao wanne wakifungiwa kucheza ligi kwa msimu miwili 201/2018 na
2018/2019 na kutozwa faini ya shilingi laki 600,000/= inayotakiwa kulipwa Juni 26 mwaka huu.


Kwa matokeo hayo Timu ya Maji Maji, MADUNGU, African Kivuymbi, Aljazira, Danger Boys na Sharp Victor zimeshuka daraja kutoka ligi kuu
ya Zanzibar kwa msimu wa 2016/2017.

No comments:

Post a Comment