Aliekuwa kocha mkuu wa
timu ya Shangani FC Kijo Nadir Nyoni amesema ameamua kuachana na mpira wa
ushindani nabadala yake kwa sasa ameelekeza nguvu zake zote katika kuimarisha
soka la vijana.
Akizungumza na zenjsport
on –line Kijo ambae kwa sasa anaifundisha katika academy ya vijana ya
blacklions football academy ya Muyuni amesema ameamua kufanya hivyo ilikuinua
vipaji vya watoto ambao kwa asilimia kubwa huishia njiani kutokana na
kukosekana kwa muendelezo wa vijana hao.
“Nimeamua kuekeza huku
katika vijana unajua Zanzibar tumejaaliwa vipaji lakini asilimia kubwa ya
vipaji hupotea kutokana na kutopatiwa msingi imara wa soka” alisema.
![]() |
Kocha wa timu ya Black lions football academy Kijo Nadri Nyoni alievaa fulana blue akielezea mikakati ya kituo chake cha black lions football academy |
Aidha Nyoni amewataka
makocha kuelekeza nguvu zao katika kuimarisha soka la vijana kwani huko ndiko
kunakoanzia kuzalisha vipaji vya soka.
“Unajua kumekuwa na
tabia kwa walimu kupenda kufundisha ngazi za juu nakuacha timu zetu za vijana
jambo ambalo linarejesha nyuma maendeleo ya soka la vijana wetu ,hivyo
ninawashauri walimu wenzangu waangalie na huku katika soka la vijana ili
kusogeza mbele maendeleo ya soka la vijana”alisema Nyoni.
![]() |
Wachezaji wa timu ya Black lions academy wakiwa katika mazoezi yakueka mwili sawa. |
Ameongeza kuwa endapo
timu za vijana zitafundishwa na walimu wenye taaluma kutapelekea vijana hao
kupata msingi nzuri wa soka lao nakupelekea taifa kuwa na ligi bora na timu
imara ya taifa.
Akizungumzia kituo
chake cha kukuza watoto kisoka cha black lion football academy cha Muyuni kocha
huyo amesema vijana waliopo katika kituo hicho wapo vizuri huku akitarajia
kuwaendeleza vijana hao ambao ndio nguvu kazi ya taifa la baadae.
Amesema kwa sasa
katika kituo cha hicho wapo katika mikakati ya mwisho yakukamilisha ujenzi wa
mabanda ya shule ilikutoa nafasi kwa vijana wao waliopo katika kituo hicho kujipatia
hudua ya kujipatia elimu katika kituo hicho.
![]() |
Wachezaji wa Black lions football academy wakimsikiliza mwalimu wao Kijo Nadri Nyoni hayupo pichani baada ya mazoezi ya timu hiyo. |
Black lions football
academy ina timu ambazo zinashiriki katika mashindano ya vijana chini ya miaka
20 Central league,chini ya miaka 19 Juvinile na chini ya miaka 15 Juniour.
No comments:
Post a Comment