Wednesday, 4 October 2017

CHARAWE YAANZA NA KIPIGO,MIEMBENI CITY KUTUPA KARATA YAKE YA KWANZA KESHO.

Timu ya Charawe imeianza vibaya ligi kuu soka ya Zanzibar kituo cha Unguja baada yakupokea kipigo cha goli 1-0 kutoka kwa timu ya KVZ mchezo ambao umevurumishwa mnamo majira ya saa kumi alasiri katika kiwanja cha Amani mjini Unguja.

Goli lililopeka kilio kwa Charawe limefungwa na
Rafael Mwambeleko mnamo dakika ya 65 ya mchezo huo.

Na katika mchezo uliochezwa mapema mnamo majira ya saa nane mchana timu ya Kilimani City ikaibuka na ushindi wa magol 3-1 dhidi ya timu ya Kipanga.

Mabao ya City yamefungwa na Bakar Bakar Mashango dakika ya 26, Joseph Josephat Kalinga dakika ya 49 na Abdillah Seif Bausi dakika ya 85.

Bao pekee la Kipanga limewekwa nyavuni na Nassor Ali katika dakika ya 90 ya mchezo.

Ligi kuu soka ya Zanzibar kanda ya Unguja itaendelea tena kesho kwa kupigwa michezo miwili katika uwanja wa Amaan.

Saa 10 za jioni wataanza kati ya Maafande wa Polisi kwa kucheza na Miembeni City, na saa 1 za usiku watakipiga Taifa ya Jang’ombe dhidi ya Zimamoto.


No comments:

Post a Comment