Tuesday, 18 July 2017

MJINI MABINGWA ROLLING STONE,MKOKO,TIOTE WAMALIZA KAZI.

Mshambuliaji wa timu ya Miembeni City aliepo katika kombaini ya wilaya ya mjini Ibrahim Abdallah(Imu Mkoko)na kiungo wa KVZ Seif Said kila moja ametupia kambani goli moja katika ushindi wa magol 2-0 dhidi ya timu ya Fire boys katika mchezo wa fainal ya mashindano hayo uliofanyika katika uwanja wa Julious Nyerere huko Mbulu Mkoani Manyara.
Kikosi cha Combine ya Wilaya ya mjini wakiwa na kikombe walichotwaa.

Ushindi huo unakuwa ushindi wa pili mfululizo wa timu ya wilaya ya mjini baada yakutwaa ubingwa huo katika mashindano yaliyofanyika mwaka jana.
Wachezaji wa combine ya Wilaya ya mjini wakishangilia baada ya ushindi wa magol 2-0.


Mjini ambao wametwaa ubingwa wa mashindano hayo bila hata yakupoteza mchezo hata mmoja katika mashindano hayo wanatarajiwa kulakiwa na mamia ya wapenda soka mara baada yakuwasili visiwani hapa.


No comments:

Post a Comment