Wednesday, 2 August 2017

JAMHURI WASHIKA USUKANI WA LIGI KUU,TAIFA YAENDELEZA UTEJA.

Timu ya taifa ya Jang’ombe imekubali kipigo cha magol 4-1 kutoka kwa timu ya Zimamoto ikiwa ni muendelezo wa ligi kuu soka ya Zanzibar mchezo uliovurumishwa katika dimba la Amani mjini Unguja jioni ya leo.


Magoli ya washindi yamefungwa na Nyange Othman magol 2 na Ibrahim Hamad magoli 2 huku goli lakufutia machozi la timu ya Taifa likifungwa na Khamis Faki.

Na katika uwanja wa Gombani kisiwani Pemba timu ya Jamhuri imeibuka na ushindi wa magol 5-0 dhidi ya Kizimbani.


Ligi kuu soka ya Zanzibar inaendelea kesho ambapo katika kiwanja cha Amani mjini Unguja JKU itakipiga na Jang’ombe boys huku katika uwanja wa Gombani kisiwani Pemba Okapi itakipiga na Mwenge.



No comments:

Post a Comment