Licha ya Zanzibar kupokwa uanachama na shirikisho la
soka barani Afrika (CAF )vilabu vya Zanzibar vitaendelea kushiriki katika
mashindano yanayoandaliwa na shirikisho hilo tofauti na wengi walivyokuwa
wakifikiria.
Hayo yameelezwa na afisa habari wa chama cha mpira
wa miguu visiwani Zanzibar Ali Bakar wakati alipokuwa akizungumza na waandishi
wa habari hapo jana katika chumba cha waandishi wa habari uwanja wa amani mjini
Unguja.
Amesema kwa mujibu wa barua ambayo imetumwa July,20
kwa rais wa chama cha mpira wa miguu visiwani Zanzibar kutoka kwa kaimu katibu
wa shirikisho la soka barani Afrika imeeleza kuwa imefuta maamuzi ya mkutano
uliofanyika march 16 mwaka huu ambayo nikupewa unachama kamili tu na
sivyenginevyo.
Amewataka wadau wa soka na wazanzibar kwa ujumla
kuacha kusikiliza maneno ambayo huzagaa miataani nakusikiliza taarifa mabazo
zitakuwa zinatolewa na chama cha mpira wa miguu visiwani ilikujiepusha na
taarifa ambazo si sahihi.
Wakati huo huo chama cha mpira wa miguu visiwani
imepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha mjumbe wa kamati tendaji ya chama
hicho Suleiman Khamis maarufu Kamba ya Mbuzi kilicotoka asubuhi ya August 7 jijini
Dar es salam.
![]() |
Marehemu Suleiman Khamis( Kamba ya Mbuzi) wa kati kati akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati tendaji ya ZFA taifa wakati wa uhai wake |
Akizungumzia taarifa ya msiba huo
msemaji wa chama cha mpira wa miguu visiwani Ali Bakar amesema taarifa kutoka
kwa ndugu wa karibu ni kuwa marehemu Suleiman alikua akisumbuliwa na Pressure
na Sukari na kabla ya kusafirishwa kupelekwa Hospitali ya Agaghan jijini Dar es
salam, pia alilazwa Hospitali kuu ya Chake Chake Kisiwani Pemba.
Amefafanua kuwa , marehemu aliwahi
kuwa muamuzi wa mpira wa miguu wakati chama cha mpira wa miguu kikijulikana
kama EFOZA, baada ya hapo alifanikiwa kupewa nafasi ya ukatibu mkuu katika timu
ya Chipukizi ambayo kwasasa inashiriki ligi kuu soka ya Zanzibar.
Marehemu amezikwa jana saa 10:00 alaasiri huko kijijini kwao
Kengeja kisiwani Pemba.
No comments:
Post a Comment