Tuesday, 8 August 2017

MSIMU WA 2018-2019 KUANZA AUGUST SAWA NA NCHI NYENGINE DUNIANI,ZFA YAWEKA WAZI MIFUMO MIPYA YA LIGI.

Chama cha mpira wa miguu visiwani Zanzibar kupitia kwa msemaji wake Ali Bakar Ali(Cheupe) kimeweka wazi mifumo mipya itakayotumika kwa ajili ya ligi madaraja mbalimbali yanayosimamia na ZFA taifa.
 
Baadhi ya washabiki wanaojitokeza katika ligi kuu soka ya Zanzibar.
Akizungumza na waandishi wa habari afisa habari huyo amesema mifumo hiyo imekuja baada ya uongozi wa ZFA kukutana na viongozi wa vilabu vinavyoshiriki madaraja husika nakukubaliana masuala kadhaa ikiweno namna itakavyoendeshwa mifumo hiyo ya ligi.

Amesema ligi kuu soka ya Zanzibar kwa msimu wa 2017-2018 inatarajiwa kuanza kutimua vumbi lake kuanzia October 1,huku ligi daraja la kwanza taifa na la pili taifa ikitarajiwa kuanza baada yakuanza kwa msimu mpya wa ligi kuu soka ya Zanzibar taarifa yakuanza kwake itatolewa hapo baadae.
 
Kiungo Costatinyo Katepa atashiriki ligi kuu soka ya Zanzibar kwa mara ya kwanza akiwa na Miembeni City.
Kuhusu ligi kuu soka ya Zanzibar itachezwa kikanda ambapo kila kanda itakuwa na timu 14 ambapo timu nne za juu kila kanda zitashindana katika hatua ya nane bora kutafuta nafasi yakuiwakilisha Zanzibar katika mashindano ya kilabu bingwa na shirikisho barani Afrika.
Amefafanua kuwa kila kanda zitashuka timu sita nakupanda timu mbili ambapo kutapelekea msimu wa 2018-2019 kuwa na timu kumi kwa kila kanda.

Kuhusu ligi daraja la kwanza taifa afisa habari huyo amesema itajumuisha timu 16 ambazo ligi hiyo itachezwa kwa mfumo nyumbani na ugeni baada ya mfumo wa makundi kama ilivyozooleka hapo awali  na tayari vilabu vinavyoshiriki ligi hiyo tayari vimeshaorodhesha viwanja vyao vya nyumbani.

Amefafanua kuwa timu sita za chini zitashuka daraja nakucheza ligi daraja la pili taifa huku timu mbili kutoka daraja la pili taifa zitapanda daraja la kwanza taifa.

Kuhusu ligi daraja la pili taifa afisa habari huyo amesema ligi hiyo itakuwa na timu 36 ambapo ligi hiyo itachezwa kwa mfumo wa makundi ambapo zitapangwa kwenye makundi matatu na kila kundi kushuka timu tatu.



No comments:

Post a Comment