Friday, 28 July 2017

PEMBA DABI,JAMHURI ,MWENGE HAPOTOSHI GOMBANI JIONI YA LEO.



Ligi kuu soka ya Zanzibar inaendelea jioni ya leo ambapo michezo miwili inatarajiwa kusukumwa katika viwanja viwili tofauti.
 
KIKOSI CHA TIMU YA JAMHURI.
Katika kiwanja cha Amani mjini Unguja vinara wa ligi hiyo JKU inaoneshana kazi na timu ya Zimamoto, huku katika kiwanja cha Gombani kisiwani Pemba Mwenge itamenyana na Jamhuri.
 
Baadhi ya washabiki wanaofuatilia michezo ya ligi kuu soka ya Zanzibar inayoendelea visiwani hapa.
Kesho ligi hiyo mitamaliza mzunguko wake wa tisa kwa michezo miwili katika dimba la Amani kutakuwa na dabi ya Jang’ombe pale Jang’ombe boys itakapomenyana na taifa ya Jang’ombe huku katika kiwanja cha Gombani kisiwani Pemba Okapi itakipiga na Kizimbani.
Wachezaji wa Zimamoto wakipongezana katika moja ya michezo ya ligi kuu soka ya  Zanzibar.

No comments:

Post a Comment