Ligi kuu
soka ya Zanzibar inaendelea jioni ya leo ambapo michezo miwili inatarajiwa
kusukumwa katika viwanja viwili tofauti.
Katika kiwanja
cha Amani mjini Unguja vinara wa ligi hiyo JKU inaoneshana kazi na timu ya
Zimamoto, huku katika kiwanja cha Gombani kisiwani Pemba Mwenge itamenyana na
Jamhuri.
Kesho ligi
hiyo mitamaliza mzunguko wake wa tisa kwa michezo miwili katika dimba la Amani
kutakuwa na dabi ya Jang’ombe pale Jang’ombe boys itakapomenyana na taifa ya
Jang’ombe huku katika kiwanja cha Gombani kisiwani Pemba Okapi itakipiga na
Kizimbani.
Wachezaji wa Zimamoto wakipongezana katika moja ya michezo ya ligi kuu soka ya Zanzibar. |
No comments:
Post a Comment