Friday, 28 July 2017

KIPA ZANTEX ASAINI MIAKA MIWILI MIEMBENI CITY



Timu ya Miembeni City imekamilisha usajili wa mlinda mlango nambari moja wa timu ya Zantex ,Ally Rajab ambae amesaini kandarasi ya miaka miwili na timu hiyo.
 
Ally Rajab akisaini kandarasi ya miaka miwili na Miembeni City huku akishuhudiwa na aliyekuwa mkurugenzi wa ufundi wa timu Ali Muhamed.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mkuu wa habari wa timu hiyo Ali Khamis imesema usajili huo unaifanya timu hiyo iwe na walinda milango watatu ambao ni Aley Ali Suleiman,Abaas Wadi Makame na Ali Rajab alikuja kuongeza nguvu katika eneo hilo. 


Ali Rajab anakuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na Miembeni City katika kipindi hichi cha usajili ambapo wiki iliyopita walimsajili mshambuliji ya Faisal Riam Lucas (Nado) ambae amesaini kandarasi ya miaka mitatu.

No comments:

Post a Comment