Saturday, 29 July 2017

NIDHAMU NI SILAHA PEKEE MICHEZONI,,WAZIRI

Waziri wa habari utamaduni utalii na michezo wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Rshid Ally Juma amewataka wachezaji wa combine ya wialaya ya mjini kuongeza bidii ilikuimarisha vipaji walivyobarikiwa na muumba.
Waziri wa habari utamaduni ,utalii na michezo Rashid Ally Juma akizungmza na wachezaji wa timu ya combine ya wilaya ya mjini.
Waziri Rashid ameyasema hayo wakati alipokuwa akizungumza na wachezaji na viongozi wa timu hiyo huko ofisini kwake waliponda kupeleka kombe waliotwaa katika mashindano ya Rolling stone yaliyofanyika Mbuu Manyara .
Wachezaji wa combine ya wilaya ya mjini na viongozi wao wakimsikiliza waziri.

Aidha amewapongeza vijana hao kwa ujasiri wa waliouonesha katika mashindano hayo licha ya changamoto kadhaa walizokabiliana nazo wakiwa katika mashindano hayo.
Ameongeza kuwa vijana hao walionesha nidhamu ya hali juu na ndo jambo pekee lililowasaidia kuweza kutwaa Ubingwa huo.
 
Kocha mkuu wa mabingwa wa mashindano ya Rolling stone combine ya wilaya ya mjini Muhamed Seif King,mjumbe wa kamati tetandaji ZFA wilaya ya mjini Kisike wakati kati na kocha msaidizi wa timu hiyo Ramadhani Madundo wakimsikiliza waziri wa habari,utamaduni,utalii na michezo.

Mapema mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu wialaya ya mjini Unguja Hassan Haji Hamza ameiomba serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kutoa michango yao ya hali na mali pindi timu itakapokuwa na amshindano nje ya Zanzibar ilikuondoa changamoto ambazo hujitokeza.

No comments:

Post a Comment