Mashindano ya vijana ndani ya wilaya ya mjini
yamefikia tamati jana ambapo mabingwa katika madaraja mbalimbali walikabidhiwa
zawadi zao.
Akizungumza na mtandao huu mara baada yakumalizika
kwa mashindano hayo mwenyekiti wa kamati ya amshindabo hayo Khamis Machano
amesema mashindabo hayo yamekwenda vyema licha ya changamoto kadhaa mabazo
zinawakabili katika kuendesha michezo hiyo.
Akielezea changamoto ambazo wanakabilina nazo katika
uendeshaji wa michezo hiyo mwenyekiti huyo amesema uhaba wa fedha imekuwa
changamoto kubwa ambayo wanakabiliana nayo katika kuendesha mashindano hayo
sambamba na idadi ndogo ya wajumbe wanaosimamia mashindano hayo ukilinganisha
na timu ambazo zinashiriki katika michezo hiyo.
Akizungumzia suala zima la zawadi mwenyekiti huyo
amesema mashindano ya mwaka huu zawadi ya fedha imepungua ukilinganisha na
mwaka jana kutokana na shughuli mbalimbali ambazo kamati yao iliziendesha
katika kipindi cha msimu uliomalizika jana.
“Unajua zawadi ya fedha imepungua ukilinganisha na
mwaka jana kutoka na shughuli mbali mbali ambazo kamati iliendesha ,msimu huu
tuliendesha kozi ya ukocha na kamati ndio iliyogharamia kwa asilimia kubwa kozi
hiyo pia kamati ilichangia kwa asilimia kubwa timu ya vijana iliyoenda Manyara
katika mashindano ya Rolling stone jambo ambalo limepelekea kamati kupunguza
zawadi ya fedha ukilinganisha na mwaka jana”alisema.
Akizungumza vitendo vya upangaji matokeo
uliojitokeza katika mashindano ya mwaka huu mwenyekiti huyo ameelezea
kusikitishwa kwake na vitendo hivyo huku akiwaomba wanaosimamia timu za vijana
kuachana na vitendo kama hivyo kwani kunarejsha nyuma maendeleo ya soka la
vijana.
Mabingwa katika madaraja mbalimbali kwa wilaya ya
mjini ni kama ifuatavyo ,Junvinile mabingwa Gold win huku makamo bingwa wakiwa Blacksaloir,Juniour
bingwa Tothham makamo bingwa Simba FC,mashindano ya mtoanao Juvinile bingwa
Blacksaloir huku makamo bingwa akiwa New academy.
Kwa upande wa mashindano ya mtoano central bingwa ni Villa coast na kwa upande wa
mashindano ya mtoano Juniour bingwa ni Al-noour.
No comments:
Post a Comment