Mabingwa wa ligi kuu soka ya Zanzibar timu ya JKU
imefanikiwa kutwaa Ngao ya jamii baada yakuifunga timu ya Miembeni City magol
2-0 katika mtanange uliovurumishwa katika dimba la Amani mjini hapa jioni ya
jana.
Katika mchezo huo ambao ulikuwa wa ushindani na
wakuvutia nakushihudiwa na mashabiki lukuki kiwanjani hapo JKU walijipatia
magol yao kupitia kwa Salum Mussa na
Nassor Mattar.
Mchezo huo unaashiria kuanza kwa msimu mpya wa ligi
ambapo ligi kuu soka ya Zanzibar ikitarajiwa kutimua vumbi lake kuanzia October
3,kwa michezo miwili JKU wakikipiga na Mafunzo huku Jang’ombe boys wakimenyana
na KMKM.
No comments:
Post a Comment