Timu ya Jang’ombe boys
pamoja timu ya JKU wanaondoka kisiwani Unguja kuelekea Pemba asubuhi hii kwa ajili
ya michezo yao miwili ya ligi kuu soka ya Zanzibar.
Nyota hao wanaondoka
visiwani kwa Meli ya MV Mapinduzi huku hali za nyota wa timu hizo wakiwa katika
hali nzuri.
Ali Othman Kibichwa
Rais wa timu ya Jang;ombe boys amesema wanaenda kisiwani Pemba kupambana
nakutafuta alama tatu katika kila mchezo huku akisisitiza kuwa hawatazarau
mchezo hata mmoja.
Kwa upande wake katibu
wa timu ya JKU Saad Ujudi amesema wanuzeofu mkubwa na michezo ya aenda kisiwani
huko kufanya vyema huku wakihitaji kushinda katika kila mchezo ilikujieka
katika nafasi mbili za juu nakuiwakilisha nchi kimataifa.
Jang’ombe boys
wanatarajiwa kujitupa katika kiwanja cha Gombani kisiwani Pemba,July 9 kumenyana
na timu ya Mwenge kutoka Wete kaskazini mwa kisiwa cha Pemba.
Huku timu ya JKU
ikitarajiwa kujitupa katika dimba hilo hilo la Gombani kisiwani Pemba ,July 10
kumenyana na timu ya Okapi michezo yote miwili ikichezwa mnamo majira ya saa
kumi alasiri.
No comments:
Post a Comment