Wednesday, 5 July 2017

WAVU kuwapiga msasa waamuzi wake.

Katika kuhakikisha kinaendesha mashindano yake kwa uweledi na ufanisi wa hali ya juu chama cha mchezo wa wavu Zanzibar kimeandaa mafunzo kwa waamuzi wanaocheza michezo hiyo ilikutekeleza majukumu yao kwa uweledi.


Akizungumzia mafunzo hayo katibu wa chama hicho  Mwalim Yustic Mwakanjuki amesema lengo la seminar hiyo nikuwafundisha waamuzi sheria mpya za mchezo huo ambazo zinaanza kutimu kuanzia mwaka huu.

Amesema kozi hiyo ya waamuzi inatarajiwa kuchukua wiki moja ambapo inatarajiwa kuanza July 10 ambapo yataendeshwa katika ukumbi wa Polis skwash.

Ameongeza kuwa mafunzo hayo yanatarjiwa kuendeshwa na mwenyekiti wa kamati ya ufundi ya chama cha mchezo huo Ali Muhamed ambapo jumla ya waamuzi 15.

Ameeleza kuwa baada yakumalizika kwa kozi hiyo chama chao kitaendesha mafunzo kwa kama hayo kwa viongozi wa vilabu.

Amewataka wadau na wapenzi wa mchezo huo kuunga mkono jitihda zao ilikufanikisha malengo ambayo chama chao yamejiekea.

No comments:

Post a Comment