Wednesday, 5 July 2017

NMB yawapiga tafu vinara wa ligi kuu soka ya Zanzibar.

Bank ya NMB imewapatia vifaa vya kimichezo timu ya Jamhuri inayoshiriki ligi kuu soka ya Zanzibar kwa ajili ya michezo iliyosalia ya ligi kuu.
Manager wa NMB Ahmed Nassor alieva koti jeusi akimkabidhi jezi manager wa Jamhuri Abdallah Muhamed Elisha

Akizungumza na mtandao huu manager wa timu ya Jamhuri Abdallah Muhamed Elisha amesema wamefikia makubali na bank hiyo na kwa sasa timu yake itavaa jezi yenye nembo ya bank hiyo ya NMB.

Kuhusu makubaliano ambayo wamekubaliana na bank hiyo amesema kwa sasa ni mapema kuyaweka yote hadharani lakini bank hiyo itagharamia usafiri wa timu hiyo kwenda nakurudi katika michezo yake yote ya ligi kuu soka ya Zanzibar.

Sambamba na hayo pia bank hiyo imekabidhi viatu kwa ajili ya wachezaji wa timu hiyo sambamba  fulana zakuchezea katika michezo yake ya ligi kuu soka ya Zanzibar.

Amewataka wadau na washabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi kuinga mkono timu hiyo iwapo uwanjani ilikufikia malengo waliyojiekea yakutwa ubingwa wa ligi kuu soka ya Zanzibar kwa mwaka huu.



No comments:

Post a Comment