Wednesday, 5 July 2017

Jamhuri kuikabili Zimamoto bila ya mshambuliji wao hatari.

Mshambuliji hatari wa timu ya Jamhuri Khamis Abdallah Mbulu ataukosa mchezo wa ligi kuu soka ya Zanzibar kati ya timu ya Jamhuri na timu ya Zimamoto mtanange ambao utavurumishwa katika dimba la Amani mjini Unguja July,10 mwaka huu.

Kikosi cha Jamhuri kinachotarajiwa kuwasili kisiwani Unguja kesho tayari kwa michezo yake miwili ya ligi kuu soka ya Zanzibar.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na manager wa timu hiyo Abdallah Muhamed Elisha yenye maskani yake Wete kisiwani Pemba nyota huyo amepata majeraha katika mazoezi ya timu hiyo hapo jana na kwa mujibu wa report ya daktari nyota huyo anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa takribani wiki moja.

Ameongeza kuwa kikosi hicho cha vinara wa ligi kuu soka ya Zanzibar  kinatarajiwa kuondoka kisiwani Pemba asubuhi ya kesho ,July 6 ,kuja Unguja kwa meli ya Azam Sea Link na wanatarajiwa kusafiri na msafara wa wachezaji 25 na viongozi watano ambapo watafikia katika hostel za chuo cha mafunzo.


Jamhuri inaongoza ligi kuu soka ya Zanzibar wakiwa na alama 9 baada yakushinda katika michezo yake mitatu waliyocheza ,wanakuja kisiwani Unguja kucheza michezo miwili ambapo July,10 watacheza na mabingwa watetezi timu ya Zimamoto huku July 13 wakikipiga na Taifa ya Jang’ombe kabla yakurudi kisiwani Pemba .

No comments:

Post a Comment