Monday, 3 July 2017

JAMHURI KUWASILI UNGUJA JULY ,6 KUENDELEZA UBABE WAKE ,LIGI KUU SOKA YA ZANZIBAR.

Vinara wa ligi kuu soka ya Zanzibar timu ya Jamhuri kutoka kisiwani Pemba wanatarajiwa kuwasili kisiwani Unguja July 6 tayari kwa mchezo wao wa mzunguko wa nne dhidi ya timu ya Zimamoto ya Unguja mtanange ambao utavurumishwa katika dimba la Amani mjini Unguja.
Kikosi cha vinara wa ligi kuu soka ya Zanzibar timu ya Jamhuri ambacho kinatarajiwa kuwasili Unguja July 6.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kocha mkuu wa timu hiyo Abdulmutik Kiduu amesema vijana wake wapo katika hali nzuri na ari ya hali ya juu kwa ajili ya kuendelea wimbi la ushindi katika michezo iliyosalia ya ligi kuu soka ya Zanzibar.

Amesema baada ya mapumziko yakupisha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani vijana wake wameendelea na mazoezi na hamasa yakufanya vyema katika kila mchezo imekuwa ikiengezeka siku hadi siku.
Mshambuliji wa mabingwa watetezi wa ligi kuu soka ya Zanzibar timu ya Zimamoto Ibrahim Hmad Hilika alievaa  jezi manjano katika moja ya michezo ya ligi kuu soka ya Zanzibar,

Kuhusu kukabiliwa na majeruhi katika kikosi chake hicho kocha huyo amesema mpaka sasa hana majeruhi hata mmoja na vijana wake wote wapo katika hali nzuri kiafya tayari kuendeleza wimbi la ushindi katika kila mchezo ambao timu hiyo itacheza.

Jamahuri ambayo imeibuka na ushindi katika michezo yote mitatu waliyocheza mpaka sasa nakukusanya alama tisa inarudi katik mzunguko huu wa lala salama wa ligi kuu soka ya Zanzibar kuhakikisha wanaendeleza ushindi katika kila mchezo ambao timu hiyo itacheza.

Ligi kuu soka ya Zanzibar inarudi tena ulingoni Jumapili ,July 9 baada yakuenda mapumziko kwa takribani mwezi mmoja kupisha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani ambapo Jumapili michezo miwili itavurumishwa katika kiwa cha Amani mjini Unguja Taifa ya Jang’ombe watakipiga na Kizimbani huku katika kiwanja cha Gombani kisiwani Pemba Mwenge itaoneshana kazi na Jang’ombe Boys.

Huku Jumatatu July 10 ,katika kiwanja cha Amani vinara wa ligi hiyo timu ya Jamhuri itaoneshana kazi na mabingwa watetezi wa mashindano hayo timu ya Zimamoto huku katika kiwanja cha Gombani kisiwani Pemba Okapi itamenyana na JKU.


RATIBA YA LIGI KUU YA SOKA ZANZIBAR – NANE BORA TOLEO NO:2 2016/2017
SIKU
TAREHE
M
 HOME TEAM
VS
AWAY TEAM
VENUE & TIME
                                                                           4TH  ROUND
J’PILI
9/7/017
13
MWENGE
VS
JANG’OMBE BOYS
SAA 10  JIONI GOMBANI
J’PILI
9/7/017
14
TAIFA
VS
KIZIMBANI
SAA 10  JIONI AMAAN
J’TATU
10/7/017
15
OKAPI
VS
JKU
SAA 10  JIONI GOMBANI
J’TATU
10/7/017
16
ZIMAMOTO
VS
JAMHURI
SAA 10JIONI AMAAN
5TH  ROUND
ALHAMIS
13/7/017
17
MWENGE
VS
JKU
SAA 10  JIONI GOMBANI
ALHAMIS
13/7/017
18
TAIFA
VS
JAMHURI
SAA 1:00USK AMAAN
IJUMAA
14/7/017
19
OKAPI
VS
JANG’OMBE BOYS
SAA 10  JIONI GOMBANI
IJUMAA
14/7/017
20
ZIMAMOTO
VS
KIZIMBANI
SAA 10JIONI AMAAN
6TH  ROUND
J’TATU
17/7/017
21
MWENGE
VS
ZIMAMOTO
SAA 10  JIONI GOMBANI
J’NNE
18/7/017
22
OKAPI
VS
TAIFA
SAA 10  JIONI GOMBANI
J’NNE
18/7/017
23
JKU
VS
KIZIMBANI
SAA 10JIONI AMAAN
J’NNE
18/7/017
24
JANG’OMBE BOYS
VS
JAMHURI
SAA 1:00USK AMAAN
7TH  ROUND
IJUMAA
21/7/017
25
MWENGE
VS
TAIFA
SAA 10  JIONI GOMBANI
IJUMAA
21/7/017
26
JANG’OMBE BOYS
VS
KIZIMBANI
SAA 10  JIONI AMAAN
IJUMAA
21/7/017
27
JKU
VS
JAMHURI
SAA 1:00USK AMAAN
J’MOSI
22/7/017
28
OKAPI
VS
ZIMAMOTO
SAA 10  JIONI GOMBANI
8TH  ROUND
J’NNE
25/7/017
29
OKAPI
VS
JAMHURI
SAA 10  JIONI GOMBANI
J’NNE
25/7/017
30
JANG’OMBE BOYS
VS
ZIMAMOTO
SAA 10  JIONI AMAAN
J’TANO
26/7/017
31
MWENGE
VS
KIZIMBANI
SAA 10  JIONI GOMBANI
J’TANO
26/7/017
32
JKU
VS
TAIFA
SAA 10JIONI AMAAN
9TH  ROUND
J’MOSI
29/7/017
33
ZIMAMOTO
VS
JKU
SAA 10  JIONI AMAAN
J’MOSI
29/7/017
34
JAMHURI
VS
MWENGE
SAA 10  JIONI GOMBANI
J’PILI
30/7/017
35
OKAPI
VS
KIZIMBANI
SAA 10  JIONI GOMBANI
J’PILI
30/7/017
36
JANG’OMBE BOYS
VS
TAIFA
SAA 1:00USK AMAAN
10TH  ROUND
J’TANO
02/8/017
37
KIZIMBANI
VS
JAMHURI
SAA 10  JIONI GOMBANI
J’TANO
02/8/017
38
TAIFA
VS
ZIMAMOTO
SAA 10  JIONI AMAAN
ALHAMIS
03/8/017
39
OKAPI
VS
MWENGE
SAA 10  JIONI GOMBANI
ALHAMIS
03/8/017
40
JKU
VS
JANG’OMBE BOYS
SAA 10JIONI AMAAN
11TH  ROUND
J’TATU
07/8/017
41
JAMHURI
VS
TAIFA
SAA 10  JIONI GOMBANI
J’NNE
08/8/017
42
ZIMAMOTO
VS
MWENGE
SAA 10  JIONI AMAAN
J’NNE
08/8/017
43
JANG’OMBE BOYS
VS
OKAPI
SAA 1:00USKAMAAN
J’NNE
08/8/017
44
KIZIMBANI
VS
JKU
SAA 10JIONIGOMBANI
12TH  ROUND
IJUMAA
11/8/017
45
JAMHURI
VS
JKU
SAA 10  JIONI GOMBANI
IJUMAA
11/8/017
46
ZIMAMOTO
VS
OKAPI
SAA 10  JIONI AMAAN
IJUMAA
11/8/017
47
JANG’OMBE BOYS
VS
MWENGE
SAA 1:00USK AMAAN
J’MOSI
12/8/017
48
KIZIMBANI
VS
TAIFA
SAA 10  JIONI GOMBANI
13TH  ROUND
J’NNE
15/8/017
49
JAMHURI
VS
ZIMAMOTO
SAA 10  JIONI GOMBANI
J’NNE
15/8/017
50
JKU
VS
OKAPI
SAA 10  JIONI AMAAN
J’TANO
16/8/017
51
KIZIMBANI
VS
JANG’OMBE BOYS
SAA 10  JIONI GOMBANI
J’TANO
16/8/017
52
TAIFA
VS
MWENGE
SAA 10JIONI AMAAN
14TH  ROUND
J’MOSI
19/8/017
53
JAMHURI
VS
JANG’OMBE BOYS
SAA 10  JIONI GOMBANI
J’MOSI
19/8/017
54
JKU
VS
MWENGE
SAA 10  JIONI AMAAN
J’PILI
20/8/017
55
KIZIMBANI
VS
ZIMAMOTO
SAA 10  JIONI GOMBANI
J’PILI
20/8/017
56
TAIFA
VS
OKAPI
SAA 10JIONI AMAAN



No comments:

Post a Comment