Mkurugenzi wa ufundi
wa timu ya Miembeni City ambayo itashiriki ligi kuu soka ya Zanzibar kwa mara
ya kwanza katika msimu ujao wa ligi Ali Mohammed ameachia nafasi hiyo aliyokuwa
akiishikilia kwa takribani miaka miwili sasa.
Akizungumza na mtandao
huu juu ya sababu ambayo imemfanya kuachia nafasi hiyo aliekuwa mkurugenzi wa
ufundi wa timu hiyo amesema ameamua kuacha nafasi hiyo ilikulinda matakwa ya
katiba ya timu yao hiyo.
“Nimeachia nafasi hii
ilikuendana na matakwa ya katiba ya timu yetu ,unajua katiba ya timu yetu
inasema nafasi ya mkurugenzi wa ufundi ni nafasi yakuajiriwa hivyo nimeachia
ili kutoa fursa kwa wenye sifa pale itakapotangazwa nafasi sambamba na kukidhi
mahitaji ya katiba yetu”aliseama.
Sambamba na hayo
amesema kwa kipindi kirefu alikuwa akivaa kofia mbili katika timu jambo ambalo ni
kinyume na katiba ya timu hiyo hivyo kuachia nafasi hiyo kutoa fursa yakubakia
na nafasi yake yakuwa mjumbe wa bodi ya wakurugenzi wa timu hiyo.
Amewaomba walimu wenye
sifa kujitokeza kuomba nafasi hiyo pale itakapotangazwa ilikuendeleza maendeleo
ya timu hiyo.
No comments:
Post a Comment