Sunday, 30 July 2017

Mwenyekiti Cetral wilaya ya mjini aachie ngazi kwa kukeuka kanunu ya mashindano ya vijana,,Real Kids.

Kamati tendaji ya timu ya Real Kids FC inayoshiriki ligi madaraja ya vijana central league wilaya ya mjini imemtaka mwenyekiti wa kamati inayosimamia mashindano ya vijana Khamis Machano kuachia nafasi hiyo baada yakukeua kanuni inayoendesha mashindano hayo.
Viongozi wa  Real Kids FC wakizungumza na waandishi wa habari.

Hayo yameelezwa na msemaji wa timu hiyo Tarik Khamis Ali wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari nakusema kuwa kitendo cha ukeukwaji wa kanuni uliofanywa na mwenyekiti huyo akishirikiana na wajumbe wa kamati yake nikurudisha nyuma juhudi za vijana waliojitolea kuimarisha vipaji vya vijana wenzao.

Amesema timu yao ilituma rufaa kwa mujibu wa kanuni inayoendesha mashindano hayo lakini mwenyekiti huyo ameshindwa kusitisha utoaji wa zawadi kwa upande wa ligi ya mtoano  century league ambayo timu ya Real Kids kupisha kusikilizwa kwa rufaa yao.

Amesema kuwa kamati ya century imekaa kutoa maamuzi bila yakuwasikiliza jambo ambalo nikinyume na taratiabu lakini jambo lakusikitisha zaidi kamati hiyo imeshindwa kuheshimu rufaa yao waliyoikata kwa kamati ya mashindano ya vijana taifa na nakala yake kupeleka kwa kamati yake lakini wakashindwa kueheshimu rufaa hiyo jambo amablo linaashirikia kushindwa kuiheshimu kanuni ya mashindano kama ilivyoorodheswa katika kifungu cha 20 C.

Ameelezea kusikitishwa kwake nakuchafuliwa kwa timu yao kwa madai yakupanga matokeo jambo ambalo si sahihi kwani hakuna ushahidi wowote ule unaoashiria vitendo vya upangaji wa matokeo.

 Amewaomba waandishi wa habari kuacha kuichafua timu yao kwa kuchukua taarifa za upande mmoja na badala yake wasikilize maelekezo kwa pande zote mbili ilikutoa taarifa iliyo sahihi.


No comments:

Post a Comment