Kamati tendaji ya timu ya Real Kids FC inayoshiriki
ligi madaraja ya vijana central league wilaya ya mjini imemtaka mwenyekiti wa
kamati inayosimamia mashindano ya vijana Khamis Machano kuachia nafasi hiyo
baada yakukeua kanuni inayoendesha mashindano hayo.
![]() |
Viongozi wa Real Kids FC wakizungumza na waandishi wa habari. |
Hayo yameelezwa na msemaji wa timu hiyo Tarik Khamis
Ali wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari nakusema kuwa kitendo
cha ukeukwaji wa kanuni uliofanywa na mwenyekiti huyo akishirikiana na wajumbe
wa kamati yake nikurudisha nyuma juhudi za vijana waliojitolea kuimarisha
vipaji vya vijana wenzao.
Amesema timu yao ilituma rufaa kwa mujibu wa kanuni
inayoendesha mashindano hayo lakini mwenyekiti huyo ameshindwa kusitisha utoaji
wa zawadi kwa upande wa ligi ya mtoano century league ambayo timu ya Real Kids kupisha
kusikilizwa kwa rufaa yao.
Amesema kuwa kamati ya century imekaa kutoa maamuzi
bila yakuwasikiliza jambo ambalo nikinyume na taratiabu lakini jambo
lakusikitisha zaidi kamati hiyo imeshindwa kuheshimu rufaa yao waliyoikata kwa
kamati ya mashindano ya vijana taifa na nakala yake kupeleka kwa kamati yake lakini
wakashindwa kueheshimu rufaa hiyo jambo amablo linaashirikia kushindwa
kuiheshimu kanuni ya mashindano kama ilivyoorodheswa katika kifungu cha 20 C.
Ameelezea kusikitishwa kwake nakuchafuliwa kwa timu
yao kwa madai yakupanga matokeo jambo ambalo si sahihi kwani hakuna ushahidi
wowote ule unaoashiria vitendo vya upangaji wa matokeo.
Amewaomba waandishi
wa habari kuacha kuichafua timu yao kwa kuchukua taarifa za upande mmoja na
badala yake wasikilize maelekezo kwa pande zote mbili ilikutoa taarifa iliyo
sahihi.
No comments:
Post a Comment