Kamati inayosimamia
soka la ufukweni visiwani Zanzibar wanatarajiwa kukutana na waziri wa habari utamaduni
utalii na michezo lengo ikiwa ni kujadili masuala kadhaa yanayohusu soka hilo
la ufukweni.
Akizungumza na
mtandao huu mwenyekiti wa kamati hiyo ya soka la ufukweni Ali Sharif Adolf
amesema ameona haja yakukutana na waziri anaehusiana na michezo,ZFA
taifa,baraza la michezo sambamba na wadau wengine wa michezo ilikuimarisha
mchezo huo wa ufukweni.
Ameongeza kuwa
katika miaka mitatu tokea kuazishwa kwa kamati hiyo ya soka la ufukweni
mafanikio kadhaa yamepatikana ikiwemo kukua kwa mchezo huo sambamba na kuchezwa
kwa mchezo wa kirafiki wa kimataifa kati ya timu ya Zanzibar ya na ile ya
Uganda.
Amewataka wadau
mbali mbali wa soka nchini kujitokeza kwa wingi katika kuimarisha mchezo huo wa
soka la vijana nakuitangaza Zanzibar kimataifa.
No comments:
Post a Comment