Saturday, 10 June 2017

Tuelekezeni duwa zetu kwa vijana wetu waliopo Mwanza,asema mwalimu Othman.

Baadhi ya wadau wa soka visiwani Zanzibar wameelezea kufurahishwa kwao na mwenendo nzuri wa timu ya soka ya kanda ya Unguja iliyopo katika mashindano ya Michezo na Sanaa ya Skuli za Sekondari Tanzania (UMISSETA) yanayoendelea katika viwanja vya Chuo cha Ualimu Butimba mkoani Mwanza.
 
Wanamichezo mbali mbali wakiwa katika maandamano ya uzinduzi wa mashindano ya UMISETA.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wadau hao wamesema wanafurahishwa na kile kinachofanywa na wanandinga hao huku wakijua wanashiriki mashindano hayo wakiwa katika wakati mgumu kutokana na asilimia kubwa ya vijana hao wanashiriki katika michezo hiyo wakiwa na funga.

Mwalimu Othman Hamad Bakari mwalimu wa michezo skuli ya Mtoni ameuambia mtandao huu kuwa yeye binafsi anafurahishwa na matokeo mazuri ambayo vijana hao wanayapata nakuwaomba wadau wa soka kuwaombea vijana hao ilikufanya vyema zaidi nakuja na kikombe cha michezo hiyo.

“Ni mwanzo nzuri ,timu imeshinda katika michezo miwili tena kwa wastani nzuri tu wa magol yakufunga jambo la muhimu kwetu nikuwaombea vijana wetu warudi na ushindi wanacheza katika mazingira magumu sana, najua asilimia kubwa ya wanamichezo wetu wapo katika mfungo “alisema mwalimu huyo.

Vijana wa kanda ya Unguja watajitupa dimba leo hii Jumamos June,10 mnamo majira ya saa sita na nusu za mchana kumenyana na Mara,ambapo vijana hao wanajitupa katika mchezo huo wakiwa na rekodi nzuri ya ushindi katika michezo iliyopita ambapo waliifunga Katavi 4-0, Kagera 3-0 wanahitaji ushindi katika mchezo wa leo ilikusonga mbele katika hatua nyengine.

Kikosi cha kanda ya Unguja  kilichopo  Mwanza katika mashindano ya UMISETA.


Michezo mengine kwa upande wa timu ya soka ya kanda ya Unguja ukiachia ule wa mchana wa leo dhidi ya Mara mnamo majira ya saa 6:30 za mchana wa leo ni ule wa Jumapili June 11, 2017 dhidi ya Mbeya, Jumatatu June 12, 2017 Unguja dhidi ya Iringa, Jumanne June 13, 2017 Unguja watamalizana na Dar es salam.

Huku kikosi cha kanda ya Unguja kikiwakilishwa na  walinda milango Aley Ali Suleiman (Ubago) na Ali Makame (Muembe ladu).

Huku kwa upande wa walinzi wakijumuishwa na Ibrahim Abdallah Hamad (Arahman), Abdurahman Seif Bausi (Glorious), Abubakar Khamis (Bububu), Abdul aziz Ameir Khatib (Arahman), Ali Issa Omar (Lumumba),  Ahmed Mohd Shaaban (Nyuki) na Abbas Yahya.

Kwa upande wa viungo kikosi hicho kinaundwa  Amani Ali Suleiman (Kiembe Samaki), Ibrahim Faraj “Mess” (Lumumba), Haji Suleiman (JKU Mtoni), Yakoub Kiparo (Langoni), Jamali Ali Jaku “Ozil” (Kinuni) na Eliyasa Suleiman (K-pura).

Huku safu ya washambuliaji ikiwajumuisha Faki Kombo (JKU Mtoni), Mundhir Abdallah (JKU Mtoni), Ali Hassan (Bububu), Walid Abdi “Pato” (Mwera), Ali Mohd Seif (Tumekuja) na Ali Omar (Mwera).







No comments:

Post a Comment