Friday, 9 June 2017

Taifa ya Jang'ombe,Gullion FC kunogesha sherehe za Idd.



Katika kuhakikisha wanafanya vyema katika msimu ujao wa ligi timu ya Gulio FC inyoshiriki ligi daraja la pili wilaya ya mjini Unguja inaendelea na mipango yake yakuimarisha kikosi chao hicho.

Washabiki wa taifa ya Jang'ombe


Akizungumza na mtandao huu rais wa timu hiyo Ahmed Khamis amesema timu yao inaendelea na mazungumzo na nyota kadhaa ambao wataongeza nguvu katika kikosi chao hicho.

Amesema kuwa kutokana na mipango ya mwalimu timu hiyo inatarajiwa kuanza mazoezi rasmini yakujiandaa na msimu ujao wa ligi Jumatatu June 12.
 
Wachezaji wa Guluion wakishangiria katika moja ya michezo ya ligi daraja la pili wilaya ya mjini katika msimu uliopita.
Aidha ameongeza kuwa katika kuonesha wanawajali wapenzi wa timu hiyo timu yao itakipiga mchezo wa kirafiki na timu ya taifa ya Jang’ombe mtanange ambao utapingwa siku ya Idd pili katika uwanja wa Amnai Mjini Unguja huku mipango kwa ajili ya mchezo huo wa kirafiki yakiendelea  vizuri.

Amefafanua kuwa kutokana na report ya mwalimu tayari uongozi umejua matatizo yaliyopelekea kutokufanya vyema katika timu yao na tayari uongozi wa timu wanayafanyia kazi mapungufu hayo.

No comments:

Post a Comment