Kituo cha
kukuza vipaji vya michezo Zanzibar(ZFDC) wanaendelea na mipango yao
yakuendeleza vipaji vya michezo kwa vijana wakizanzibar ambapo asubuhi ya kesho
wanatarajiwa kuendesha mchujo kwa ajili ya nyota wapya watakaojumuika katika
kituo hicho.
Akizungumza
nasi mkurugenzi wa kituo hicho Omar Bakar amesema wanatarajiwa kukusanya vijana
wa chini ya miaka 12 mpaka 20 ambapo katika mchujo wao wa hapo kesho wamepanga
kukusanya vijana ambao watakuwa na uwezo wa hali ya juu yakusakata soka.
Ameongeza kuwa
katika kituo chao hicho ambacho kinatarajiwa kukusanya jumla ya nyota 50 ambao
watakuwa na umri wa chini ya miaka 20 kina lengo lakuimarisha soka la vijana
katika kisiwa cha Unguja.
Aidha amewaomba
wazazi kujitokeza kuwapeleka watoto wao kujaribu bahati yao ilikujumuika na
nyota waliopo katika kituo hicho.
No comments:
Post a Comment