Saturday, 1 July 2017

Taifa ya Jang’ombe,Dulla Boys kuipa mazoezi Combine ya Rolling Stone.


Kikosi cha combine ya wilaya ya mjini kinaendelea na maandalizi yake kujiandaa na mashindano ya Rolling Stone yanayotarajiwa kufanyika July 9 hadi 19,Mbulu Manyara.
 
Timu ya taifa ya Jang'ombe.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na katibu wa chama cha mpira wa miguu wilaya ya mjini Unguja Yahya Juma kikosi hicho kinaendelea na maandalizi na kinatarajiwa kucheza michezo miwili ya mwisho ya kirafiki kabla yakuondoka July 6 kuelekea katika mashindano hayo.

Amesema michezo hiyo ya kirafiki ni ule utakaovurumishwa kesho July 3 mnamo majira ya saa kumi alasiri ambapo combine hiyo itamenyana na timu ya Dulla boys sambamba na ule wa July 5 ambapo timu hiyo itajipima nguvu na timu ya Taifa ya Jang’ombe.
 
Wachezaji wa combine ya wilaya ya mjini.
Amesema kikosi cha wachezaji 20,na viongozi 5 wanatarajiwa kuondoka July ,6 kuelekea katika mashindano hayo ambapo mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu wilaya ya mjini Hassan Haji Hamza akitarajiwa kuongoza kikosi hicho kuelekea katika mashindano hayo.


1 comment:

  1. Wadau wa soka please tuichangie timu yetu hii ikatuwakilishe kwa vizuri na kuitangaza Zanzibar nje ya mipaka yake

    ReplyDelete