Kamati ya uchaguzi ya
chama cha mpira wa kikapu visiwani imeghairisha uchaguzi uliokuwa ufanyike
asubuhi ya jana ambao ungepelekea kupatikana kwa viongozi watakaongoza mchezo
wa kikapu katika wa wilaya ya mjini kwa kipindi cha miaka minne ijayo.
Akitolea ufafanuzi juu
yakuhairishwa kwa uchaguzi huo katibu wa kamati ya uchaguzi Kibabu Hajji Hassan
amesema wameamua kuhairisha uchaguzi huo kutokana nakutokukamilika kwa idadi
inayotakiwa ya wajumbe ambao wanasifa zakupiga kura.
Amesema kuwa kwa
mujibu wa mrajisi wa vyama vya michezo vilabu ambavyo vimefanyiwa usajili ni 20
huku waliohudhuria katika uchaguzi huo vikiwa 6 tu jambo ambalo kwa mujibu wa
katiba itakuwa havijafikia matakwa ya katiba katika kuendesha zoezi hilo.
Ameongeza kuwa katika
vilabu sita vilivyohudhuria katika zoezi hilo ,vilabu vitatu havikukamilisha
taratibu za kisheria jambo ambalo lingepelekea kupatika kwa viongozi kinyume na
sheria nakulazimika kusitisha zoezi hilo la uchaguzi.
Kwa upande mwengine kibabu
amesema wao hutakiwa kutoa taarifa za uchaguzi kwa wilaya mara baada ya kupokea
maelekezo kutoka kwa kamati tendaji iliyomaliza muda wake nakutokuhudhuriwa na
wajumbe stahiki katika zoezi hilo wao kama kamati hawahusiki na sakata hilo.
Kwa upande wake katibu
wa timu ya KVZ Mtumwa Abdallah Silima amesema kuhairishwa kwa uchaguzi huo imewaathiri kidogo na suala hilo linatokana na
ucheleweshaji wa ufikishwaji taarifa kwa
wakati.
No comments:
Post a Comment