Katika
kuhakikisha anatoa michango yake katika kuendeleza maendeleo ya soka la
Zanzibar Rais wa timu ya Miembeni City Seif Kombo (Seif Bosi)asubuhi ya leo
ametoa mchango wake kwa timu ya Combine ya wilaya ya mjini inayotarajiwa
kuelekea Mbuli mkoani Manyara baada yakumalizka kwa mfungo wa mwezi mtukufu wa
Ramadhani.
![]() |
Mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu wilaya ya mjini Unguja Hassan Haji alieva kapelo akipokea fedha kwa rais wa timu ya Miembeni City Seif Kombo. |
Rais wa
Miembeni City alikabidhi mchango wake huo kwa mwenyekiti wa ZFA Wilaya ya mjini
Unguja Hassan Haji(Chura) mara baada yakumalizika kwa mazoezi ya vijana hao
yanayoendelea kila siku katika kiwanja hicho.
Akipokea
mchango huo mwenyekiti huyo amemshukuru rais huyo nakuwataka wadau mbali mbali
wa soka kuunga mkono kikosi hicho ilikufanikisha safari yakuenda kulitetea taji
hilo walilotwaa katika mashindano yaliyopita.
![]() |
Kocha wa timu ya combine ya wilaya ya mjini Muhamed Seif King akizungumza na wachezaji wa timu hiyo baada ya mazoezi. |
Ameongeza
kuwa bado timu hiyo inahitaji michango ya hali na mali ilikufanikisha safari ya
mabingwa hao watetezi wa mashindano hayo.
Kikosi cha
combine ya wilaya ya Mjini kiundwa na walinda milango Alley Ally(Miembeni City)Makkame
Mikidadi(Huru)Peter Dotto(Schake 04) walinzi Muharamami
Khamis(Blacksaloir)Abdulkhamid Salum(KVZ)Ali Hassan(Uhamiaji)Hassan
Haji(Kipanga)Ismail Mchana(Mwembebeni)Abubakary Ame(Miembeni City)Ali
Juma(Taifa ya Jang’ombe)Shaaban Pandu(Villa United)
Wengine
Yakoub Amour(Jang’ombe Boys),Ibrahim Ali(Villa Central)Suleiman Ali(Jang’ombe
boys)Mussa Shaaban Vicent(Zimamoto)Muhamed Haji(Jang’ombe boys)Muhamed
Mussa(Mapembeani)Talib Hamad(Kipanga)Seif Said (KVZ)Fahmi
Salum(Mlandege)Abdurahama Juma(KMKM)Muhamed Jailan(Chriss fc)Juma Ali (Villa
United)Suleiman Ali(Uhamiaji)Ibrahim Abdallah(Miembeni City)Muhamed
Ridhaa(Villa United)
No comments:
Post a Comment