Saturday, 10 June 2017

POLISI WAJIPANGA KUTWAA UBINGWA LIGI KUU YA KIKAPU.



Mabingwa wa mashindano ya  karume cup kwa upande wa mpira wa kikapu timu ya polisi ya zanzibar imepania kufanya vizuri katika michezo ya ligi kuu ya Zanzibar kwa mchezo huo.
 

Akizungumza na mtandao huu msemaji wa timu hiyo Hamid Fadhil amesema baada yakukamilika kwa mashindano ya ya Karume cup na timu yao kutwaa ubingwa  kwa sasa wanajipanga kukisuka kikosi chao hicho.

Amesema kuwa tayari kamati ya usajili ya timu hiyo imeshakutana na viongozi wao ilikupanga masuala kadhaa yanayohusu usajili huku wakitarajia kuwajumusiha nyota kadhaa wapya katika kikosi chao hicho.


Kuhusu mashindano ya karume cup msemaji huyo amesema mashindano hayo yanahamasa kubwa na kutwaa ubingwa katika michezo hiyo kunazidi kuamsha hamasa kwao.

Amewataka wadau na wapenzi wa timu hiyo kuendelea kuwaunga mkono ilikuweza kufanya vyema katika mashindano hayo ya ligi kuu ya mchezo huo kwa upande wa kanda ya Unguja.


No comments:

Post a Comment