Na Ramadhani Ali – Maelezo Zanzibar.
Mradi wa Kuimarisha huduma za Afya Zanzibar (HIPZ) unatarajia
kukusanya zaidi ya dola za Marekani 25,000 kwa ajili ya kusaidia huduma za afya
katika Hospitali ya Makunduchi na Kivunge ambazo wanazisaidia.
![]() |
Washiriki wa resi za baskeli (Bike Ride 2017) wakikata maeneo ya viwanja vya Maisra kuendelea na safari yao itakayochukua siku sita. Picha na Makame Mshenga. |
Fedha hizo zitapatikana
kufuatia kuandaa resi za baiskeli za kilomita 300 (Bike Ride 2017) katika mikoa
mitatu ya Unguja yatakayo dumu kwa muda wa siku sita kuanzia leo.
Akizungumza na waandishi wa
habari Hoteli ya Tembo, Mratibu wa resi hizo Dkt. Jon Rees kutoka Uingereza
amesema jumla ya wapanda baiskeli 25 kutoka Ulaya na Zanzibar
wanashiriki.
![]() |
Mratibu wa resi za baskeli (Bike Ride 2017) Dkt. Jon Rees akizungumza na waandishi wa habari kuhusu dhamira ya mbio hizo Zanzibar ikiwa ni mara yake ya tatu. Picha na Makame Mshenga |
Amesema fedha hizo zitachangwa na makampuni ya ndani na nje ya
nchi na zitatumika kuimarisha huduma za afya hasa afya ya mama na
mtoto katika Hospitali za Kivunge na Makunduchi.
Amesema Resi hizo ambazo ni
mara ya tatu kufanya Zanzibar zilianzia Mji Mkongwe kuzunguka maeneo
mbali mbali ya Mkoa Mjini Magharibi zitapitia Nungwi, Makunduchi, Kizimkazi na
zitrejea Mji Mkongwe.
![]() |
Picha ya pamoja ya washiriki wa Bike Ride 2017 wakifurahia mbio hizo kabla ya kuanza rasmi. Picha na Makame Mshenga |
Dkt. Ress amewataka wananchi
wa Zanzibar kuwaunga mkono na kuwatia hamasa wapanda baiskeli hao hasa katika
sehemu watakazopita.
Akizindua resi hizo,
Mkurugenzi Kinga na Elimu ya Afya Dkt. Fadhil Abdalla Mohd amesema Mradi wa
HIPZ umeleta mafanikio makubwa katika ubunifu wake wa kutafuta fedha kwa
ajili ya huduma za afya kwa kuanzisha mbio hizo.
No comments:
Post a Comment