Sunday, 11 June 2017

Vijana 30,wajumuishwa ZFDC.



Jumla ya vijana 30 wamefanikiwa kupata nafasi yakujiunga na kituo cha kukuza vipaji vya michezo Zanzibar(ZFDC) katika zoezi lakutafuta vijana hao lililofanyika asubuhi ya leo katika uwanja wa Amani mjini Unguja.

 
Zoezi hilo lakusaka vipaji lilisimamiwa na makocha kadhaa wa mpira visiwani na vijana waliobahatika kupata nafasi yakujiunga katika kituo hicho watapatiwa hudu zote za msingi ambazo zinahitajika kwa wanamichezo.

Akizungumza na mtandao huu manager wa kituo hicho cha kukuza vijana Omar Bakar amesema vijana hao 30 ambao wamewapata leo watajumuika na wengine watakaopatikana katika zoezi kama lililofanyika asubuhi ya leo wiki ijao.

 Ameongeza kuwa lengo la kituo chake hicho nikukusanya jumla ya vijana 50 wenye miaka chini ya umri 20 lengo nikuwajengea misingi imara yakucheza mchezo wa soka.

No comments:

Post a Comment