Friday, 18 August 2017

Umaliziaji ndio tatizo kwetu ,Mayanja..Simba yalazimishwa sare na Mlandege.

 Kocha msaidizi wa timu ya Simba Mayanja amesema umaliziaji umekuwa tatizo katika kikosi chao jambo ambalo kwa sasa mwalimu analifanyia kazi kwa nguvu zote.

Kocha huyo ameyasema hayo baada ya sare yakutokufunga na timu ya Mlandege ikiwa ni miongoni mwa michezo ya kirafiki kwa timu hiyo iliyopo kisiwani kujiandaa na mchezo wa ngao ya hisani dhidi ya Yanga.


Amesema licha yakutengeneza nafasi kadhaa lakini bado safu yake ya usambuliaji inaoneka haipo makini sana hivyo wanazitumia simu hizi zilizosalia kurekebisha matatizo hayo.


No comments:

Post a Comment