Thursday, 17 August 2017

Miembeni City yaanika nyota wake wapya,yaanza kujinoa kwa ajili ya ligi.

Kikosi cha Miembeni City kimeanza rasmini maandalizi ya msimu mpya wa ligi chini ya kocha Muhamed Seif King katika kiwanja cha Amani mjini hapa.
Mlinzi wa kati wa timu ya Miembeni City Abdullatif Juma Tiago aliesajiliwa msimu huu akitokea Criss.

Kikosi hicho ambacho kwa mara ya kwanza kitashiriki ligi kuu soka ya Zanzibar kwa msimu huu kimeongeza sura mpya kumi.
Ali Bausi mchezaji aliesajiliwa Miembeni City akitokea Muembeladu.

Akizungumza na waandishi wa habari mkuu wa kitengo cha habari wa timu hiyo Ali Khamis Ibny amesema wamefanya usajili kulingana na matakwa ya mwalimu mkuu wa timu hiyo sambamba na ligi husika.

Akiwataja nyota hao ambao wameongezwa katika kikosi hicho ni pamoja na walinda milango Ali Rajab kutoka Zantex na George Munish ambae ni mchezaji huru.
Ali Rajab mlinda mlango wa Miembeni City aliesajiliwa akitokea Zantex.

Pia timu imewasajili walinzi Abdullatif Juma Tiago kutoka Criss,Halid Bofu kutoka Twalipo academy Dar es salam, Nassoro Abdallah ,Abdallah Heri wote kutoka United Mtoni,
Nassoro Abdallah mwenye kusubiri mpira na ,Abdallah Heri ambao ni miongoni mwa nyota wapya wa Miembeni City waliotokea United Mtoni,
Wengine ni Muhamed Jeilani Msuva kutoka Criss, Ali Bausi kutoka Muembeladu,Feisal Lucas Nado kutoka Chukwani United na Muhamed Abdallah Banka JKU.
Muhamed Banca nyota mpya wa Miembeni City aliyesajiliwa akitokea JKU.

Aidha amesema kwa mujibu wa mipango ya mwalimu kikosi hicho kitacheza michezo minne ya kirafiki yakujieka sawa kwa ajili ya mfumo mpya wa ligi.
Kocha mkuu wa timu ya Miembeni City Muhamed Seif King akizungumza na wa timu hiyo baada ya amzoezi ya asubuhi.

Miembeni City ambayo itashiriki ligi kuu soka ya Zanzibar kwa mara ya kwanza imepania kuona inafanya vyema katika ligi hiyo.


No comments:

Post a Comment