Wednesday, 16 August 2017

Simba kujipima na Mlandege, kesho.

Timu ya Simba SC ambao wapo Visiwani Zanzibar kwaajili ya kuweka kambi hadi Agost 22, 2017, kesho Alhamis watacheza mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Mlandege SC mchezo ambao utasukumwa majira ya saa 2:00 za usiku katika uwanja wa Amaan.


Mlandege ambao wamepanda daraja kutoka la pili wilaya ya mjini hadi la pili taifa ambalo watacheza msimu ujao kwa sasa imekuwa moja kati ya timu zenye kufanya vyema katika soka la Zanzibar lengo nikurejesha hadhi ya timu hiyo iliyokuwanayo katika miaka ya 90.



Huu ni mchezo wa kwanza kwa timu ya Simba kucheza Visiwani hapa ndani ya msimu huu mpya ambapo pia itakuwa ni mchezo wake wa tano wa kirafiki kufuatia kucheza michezo minne.

No comments:

Post a Comment