Tuesday, 15 August 2017

Simba yaanza kujifua Zenj bila Bocco.

Kikosi cha Simba asubuhi ya leo kimeanza mazoezi yake visiwani Zanzibar kujianda na michezo ya ligi kuu soka ya Vodacom sambamba na mchezo wa Ngao ya jamii dhidi ya Yanga unaotarajiwa kufanyika September 23 mwaka huu.

Akizungumza na mtanadao huu mara yakumaliza kwa mazoezi ya asubuhi ya leo kocha msaidi wa timu hiyo Jackson Mayanja amesema hali ya kikosi chao ipo vizuri huku wakitarajia kufanya vyema katika msimu ujao wa ligi sambamba na mchezo wao dhidi ya mahasimu wao wa jadi.


Akizungumzia majeruhi yaliopo katika kikosi chao hicho kocha huyo amesema Shomari Kapombe na John Boko huku wakitarajia Boko kurudi mapema uwanjani kwani tatizo lake sio kubwa sana.










No comments:

Post a Comment