MSHAMBULIAJI mpya wa Yanga, Ibrahim Hajib leo
amefunga bao lake la kwanza katika timu hiyo ikishinda 2-0 kwenye mchezo wa
kirafiki dhidi ya Mlandege Uwanja wa Amaan, Zanzibar
Pamoja na kufunga dakika ya 50 akimalizia krosi ya Mzimbabwe Donald Ngoma, Hajib pia leo ametoa pasi ya bao la pili lililofungwa na winga machachari, Emmanuel Mrtin dakika ya 73.
Baada ya dakika 45 za kipindi cha kwanza kumalizika timu hizo zikiwa hazijafungana, kocha Mzambia, George Lwandamina leo alibadilisha wachezaji wote kipindi cha pili, kasoro kipa Ramadhan Awam Kabwili.
Na ni mabadiliko aliyoyafanya ndiyo yaliipa
ushindi timu yake katika mchezo huo wa kujiandaa na mechi ya Ngao ya Jamii
dhidi ya mahasimu, Simba Agosti 23, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Akizungumzia mchezo
huo kocha wa timu ya yanga George Lwandamina amesema ameutumia mchezo kuangalia uimara wa wachezaji wake.
Nae kocha wa timu ya
Malandege Jaala Salum amesema mchezo huo wameutumia kukitengeneza kikosi chao
kuelekea msimu ujao wa ligi.
Yanga iko Zanzibar
ikiendelea na maandalizi ya kujiwinda na pambano lao la ngao ya jamii dhidi ya
Simba litakalopigwa agost 23 mwaka huu katika uwanja wa Taifa jijini Dar es
salaam ambapo asubuhi ya leo kikosi hicho kitaelekea kisiwani Pemba kwa kambi
kabla ya kurejea jijini Dar es salaam siku mbili kabla ya mchezo huo
unaotarajiwa kuwa na ushindani wa hali juu.
.
No comments:
Post a Comment