Mkuu wa
operesheni na mafunzo pamoja na michezo ndani ya jeshi la wananchi wa Tanzania Brigidia
General Alfred Kapinga amewataka
wachezaji wa timu ya majeshi ya Tanzania kuongeza bidii na nidhamu katika
mazoezi ilikufanya vyema katika mashindano ya majeshi kwa nchi za Afrika
mashariki na kati.
Hayo ameyaeleza
wakati alipokuwa akizungumza na wachezaji na viongozi wa timu hiyo katika kambi
ya wanamichezo wa majeshi iliyopo Zanzibar.
Amewataka
wanamichezo hao kujituma kwa vile michezo ni sehemu ya kazi zao huku akielezea
imani yake yakufanya vyema katika michezo hiyo.
Amesema
wameamua kuzileta timu hizo za majeshi kueka kambi visiwani Zanzibar kutokana
na mazingira yalivyo sambamba na ukarimu uliopo kwa wazanzibar.
Nao makocha
wa timu mbali mbali za majeshi wamesema wanaenda katika mashindano hayo ya
majeshi kwa nchi za afrika mashariki na kati wamesema wanaenda katika
mashindano hayo kupambana ilikutwaa ubingwa.
Mashindano ya michezo ya Majeshi kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati mwaka huu yatafanyika Bujumbura Mjini Burundi kuanzia Agost 20, 2017 ambapo timu za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) litashiriki kwa michezo mitano ikiwemo mpira wa Miguu, mpira wa Kikapu, mpira wa Wavu, mpira wa Pete na Riadha.
No comments:
Post a Comment