Thursday, 8 June 2017

GOLI LA IMU MKOKO, LAMNAWISHA USO KOCHA KING.



Goli la dakika ya 78 la mshambuliaji wa kilabu ya Miembeni City Ibrahim Abdallah(Mkoko) limepelekea sare katika mchezo wa kirafiki kati ya timu ya combine ya Rolling Stone na timu ya Dulla Boys.

Nyota wa combine ya wilaya ya mjini akiwa na mchezaji mwezake wa Jang'ombe boys.


Mchezo huo wa kirafiki uliofanyika mnamo majira ya saa mbili na nusu usiku katika dimba la Amani ulikuwa na ushindani kwa pande zote huku ukishuhudiwa kuhudhuriwa na washabiki kadhaa uwanjani hapo.

Combine ya Rolling stone ndio ya kwanza kujipitia goli kupitia kwa
Yakubu Amouri goli ambalo lilikuwa kivutio kwa washabiki waliofika katika uwanja huo kutoka na ustadi wa hali ya juu uliofanya na mlinzi.

Kuingia kwa goli hilo kulipelekea vijana wa Dulla Boys kucharukwa nakujianda magol mnamo dakika ya 48 na 65 kupitia kwa mshambuliaji wao Simai Ali ambae alikuwa kivutio katika mchezo huo kutokana nakuipa tabu safu ya ulinzi ya combine ya Rolling Stone iliyokuwa ikiongozwa na mlinzi wakati wa Miembeni City Abubakary Ame.

Rolling Stone walipata goli la kusawazisha mnamo dakika ya 78 kupitia kwa mashambuliaji wa Miembeni City Ibrahim Abdallah.

Akizungumza na mtanadao huu mara baada ya mchezo huo mshambuliji wa combine ya Rolling Stone Ibrahim Abdallahameelezea kufurahishwa kwake na kiwango alichoonesha katika mchezo huo huku akitarajia kufanya mazuri zaidi katika michezo ijayo.

Nae mfungaji wa magol mawili ya timu ya Dulla Boys Simai Ali amesema mchezo ulikuwa na upinzani huku akielezea kufurahishwa na aina ya uchezaji walionao wachezaji wa combine ya Rolling Stone.

Kikosi cha Combine ya wilaya ya mjini kinatarajiwa kuondo visiwani Zanzibar kuelekea Mbulu Manyara ,Tanzania bara July 4 mwaka huu tayari kwa ajili ya mashindano hayo.

1 comment:

  1. Hongera kocha king kwa kuonyesha uwezo wako wakuchagua vipaji na kuviunganisha pamoja

    ReplyDelete