Friday, 18 August 2017

Simba kujipima na Gulion FC usiku wa leo.

Timu ya Simba inatarajiwa kucheza mchezo mwengine wa kirafiki na timu ya Gulion mchezo ambao utavurumishwa usiku wa leo katika kiwanja cha Amani mjini Unguja.

Wachezaji wa Simba.

Simba ambayo imeeka kambi kisiwani Unguja kujiandaa na mchezo wa Ngao ya hisani dhidi ya Yanga sambamba na ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara mchezo na Gulion utakuwa mchezo wa pili wa kirafiki kisiwani hapa.

Kikosi cha Simba.

Akizungumzia mchezo huo kocha wa timu ya Gulion ambae pia aliwahi kuwa kocha wa timu ya Simba Burghani Himid  Msoma amesema mchezo huo wa kirafiki utaisaidia kikosi chao katika  kukianda kwa ajili ya msimu ujao wa ligi.
Kocha wa timu ya Gulion FC Burghani Himid  Msoma 

Amesema kuwa amekiona kikosi cha Simba na namna wanavyocheza na anatarajia mchezo wa usiku huu utakuwa na ushindani wa hali ya juu nawakuvutia.



No comments:

Post a Comment