Timu ya Simba inatarajiwa kucheza
mchezo mwengine wa kirafiki na timu ya Gulion mchezo ambao utavurumishwa usiku
wa leo katika kiwanja cha Amani mjini Unguja.
Wachezaji wa Simba. |
Simba ambayo imeeka kambi kisiwani
Unguja kujiandaa na mchezo wa Ngao ya hisani dhidi ya Yanga sambamba na ligi
kuu ya Vodacom Tanzania bara mchezo na Gulion utakuwa mchezo wa pili wa
kirafiki kisiwani hapa.
Kikosi cha Simba. |
Akizungumzia mchezo huo kocha wa
timu ya Gulion ambae pia aliwahi kuwa kocha wa timu ya Simba Burghani Himid Msoma amesema mchezo huo wa kirafiki
utaisaidia kikosi chao katika kukianda
kwa ajili ya msimu ujao wa ligi.
Amesema kuwa amekiona kikosi cha
Simba na namna wanavyocheza na anatarajia mchezo wa usiku huu utakuwa na
ushindani wa hali ya juu nawakuvutia.
No comments:
Post a Comment