Wakiwa wanaendelea kujiandaa kwa ajili ya mchezo wao dhidi ya watani wao
wa timu ya Simba usiku wakuamkia leo imejitupa katika dimba la Amani mjini
Unguja kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya Gulion FC inayoshiriki ligi daraja
la pili wilaya ya mjini Unguja.
Katika mchezo huo ambao Simba waliutawala mchezo huo kwa asilimia kubwa
wekundu hao wa msimbazi imeibuka na ushindi wa magol 5-0 magoli yaliyofungwa na
mshambuliaji Laudit mavugo katika dk ya 13 na 40, Shiza kichuya dk ya 37,Juma
luzio dk ya 41 na Mohd Ibrahim,mo akaimalizia karamu ya bao mnamo dakika ya 67.
Simba ambao wameonekana kuutawala mchezo huo kwa asilimia kubwa
nakuwazidi wapinzani wao huu utakuwa mchezo wa mwisho wa majaribio kisiwani
hapa.
Akizungumzia mchezo huo kocha msaidizi wa timu ya Simba Jackson Mayanja
amesema mchezo huo umesaidia kuona kasoro zilizopo katika kikosi chao
nakuyafanyia kazi.
Aidha amesema wamejaribu kubadilisha mfumo kwa kuchezesha washambuliaji
wawili ilikutengeneza peya kutokana na kukabiliwa na majeruhi kwa baadhi ya
nyota wao akiwemo mshambuliaji Bocco na Okwi.
Kwa upande wake kocha wa timu ya Gulion Burhan Msoma amesema wamepoteza
mchezo huo kutokana na wachezaji wake kutokuwa imara kimwili.
Simba wanatarajiwa kuondoka visiwani August 22 kuelekea Tanzania bara
tayari kuwakabili wapinzani wao Yanga mtanange ambao utavurumishwa August 23
katika uwanja wa taifa Dar es Salam.
Kikosi cha Gulioni FC kilikuwa; Haji Yussuf,
Ibrahim Hamisi, Shaaban Hassan, Mohammed Omar, Nuhu Ally, Ulele Uledi, Hamad
Kawamba, Ally Mbaraka, Ally Amour, Ally J Kipanga na Fahim Khalfan.
Simba SC; Aishi Manula/EmManuel Mseja, Erasto Nyoni, Ally Shomary/Mohammed Hussein ‘Thshabalala’, Salim Mbonde, Method Mwanjali/Paul Bundala, James Kotei/Jonas Mkude, Haruna Niyonzima/Mwinyi Kazimoto, Muzamil Yassin/Said Ndemla, Laudit Mavugo/Mohammed ‘Mo’ Ibrahim, Juma Luizio na Shiza Kichuya/Jamal Mnyate.
No comments:
Post a Comment